top of page
Search

Umuhimu wa Unywaji wa Maji Kipindi cha Baridi kwa Watoto na Wazee

  • ThriveCare Nutrition
  • Jul 9
  • 1 min read

Watu wengi husahau kunywa maji wakati wa baridi kwa sababu hawahisi kiu kama ilivyo kipindi cha joto. Hii inaweza kusababisha upungufu wa maji mwilini, jambo linaloathiri afya kwa ujumla.

Kwa nini maji ni muhimu hata kipindi cha baridi?

  • Husaidia mfumo wa mmeng'enyo kufanya kazi vizuri.

  • Huzuia kuharibika kwa ngozi na midomo kukauka.

  • Husaidia kusafisha mwili na kutoa sumu.

  • Kwa wazee, huzuia tatizo la kufunga choo na uchovu.

Vidokezo vya kuongeza unywaji wa maji:

  • Weka ratiba ya kunywa maji (kabla ya milo, baada ya kuamka, kabla ya kulala).

  • Tumia maji ya uvuguvugu kama hayapendezi baridi.

  • Wape watoto vinywaji asilia kama juisi ya matunda isiyo na sukari kwa kiasi.

  • Tumia tikiti, matango, na matunda yenye maji mengi kuongeza kiwango cha maji mwilini.


 
 
 

Recent Posts

See All

Comments


bottom of page